BAO LA MAPEMA KUMDHURU MOURINHO

PAUL POGBA

Huenda ukawa ni wakati mgumu sana kuwahi kutokea katika maisha ya kufundisha soka ya mtaalam wa ufundi Mreno Jose Mourinho baada ya kupata sare nne mfululizo katika dimba la nyumbani Old Traford.Bao la Diafra Sakho wa West Ham sekundi ya 90 dhidi ya Manchester United ni moja ya mabao ya haraka zaidi katika historia ya Ligi kuu ya Uingereza EPL. Bao hilo liliwachanganya wachezaji wa United na kupelekea kutoa sare ya 1-1 dhidi ya West Ham ambapo mechi hiyo huenda ikaacha adhabu kwa kocha Jose Mourinho.

Mourinho sasa anakabiliwa na adhabu ya kufungiwa mechi mbili baada ya kutolewa kwenye eneo lake kwa mara ya pili ndani ya mwezi mmoja. Hata hivyo pamoja na Mourinho kuwa hatihati kufungiwa bado sare hiyo ya 1-1 na West Ham United imeingia kwenye historia ikiwa ni ya nne mfululizo katika uwanja wa Old Trafford kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 36.MOURINHOMourinho aliondolewa kwenye benchi kutokana na Utovu wa nidhamu kwa mwamuzi baada ya Paul Pogba kujirusha kisha kupewa kadi ya njano ambapo Mreno huyo alidai mchezaji wake ameonewa ndipo mwamuzi wa nne Jonathan Moss alimwamuru Jose Mourinho kuondoka kwenye eneo la ufundi kuanzia dakika ya 60.

1 comment:

  1. Welcome to JamBase - JamBase at JamBase!
    JamBase 남양주 출장마사지 at JamBase! JamBase! 상주 출장샵 JamBase has over 200 different games. With over 100 slot machines, JamBase is one of the top 과천 출장샵 ones 서귀포 출장마사지 in the business and 세종특별자치 출장안마

    ReplyDelete

Adbox

@templatesyard