LEO ULAYA MOTO, ARSENAL, CHELSEA, BARCA, DORTMUND, NAPOLI, AC MILAN…!!!


RAHA NI ARSENAL v NAPOLI, STEAU v CHELSEA, PORTO v ATLETICO, CELTIC v BARCA!
MECHI za Pili za Makundi E hadi H zipo Dimbani leo huku Chelsea wakiwa Ugenini wakisaka ushindi wao wa kwanza baada ya kutandikwa katika Mechi yao ya kwanza, Arsenal wapo Emirates na mtanange mkali sana na Napoli huku Vigogo Barcelona, bila ya Supastaa Lionel Messi, wakiwa Ugenini Uwanja wa Celtic Park ambako Msimu uliopita walinyukwa.
PATA TAARIFA ZAIDI:
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumanne 1 Oktoba 2013
[Saa 1 Usiku]
Football Club Zenit v FK Austria Wien
[Zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku]
FC Basel 1893 v FC Schalke 04
FC Steaua Bucureşti v Chelsea FC
Borussia Dortmund v Olympique de Marseille
Arsenal FC v SSC Napoli
FC Porto Club v Atlético de Madrid
AFC Ajax v AC Milan
Celtic FC v FC Barcelona
KUNDI E
Basle v Schalke
Basle, ambao walifika Nusu Fainali ya EUROPA LIGI Msimu uliopita, wameanza Kundi hili kwa kishindo kwa kuitwanga Chelsea 2-1 huko Stamford Bridge kwa Bao za Mohamed Salah na Marco Streller na huo ukawa ushindi wa kwanza kwa Klabu za Uswisi Nchini England katika Mechi 20.
Mara ya mwisho Basel kukutana na Klabu ya Germany ni kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za UCL Msimu wa 2011/12 na kuchapwa 7-0 na Bayern Munich.
Basel ndio wanaongoza Ligi ya Uswisi lakini kwenye Mechi yao ya mwisho walitoka Sare 2-2 na Sion.
Schalke walishinda Mechi yao ya kwanza ya Kundi hili kwa kuichapa Steaua Bucharest 3-0 lakini kwenye Bundesliga wapo katikati kwenye Msimamo na Jumamosi iliyopita waliongoza 2-0 dhidi ya Hoffenheim na kulazimishwa Sare ya 3-3.
Kevin-Prince Boateng, Nyota wao walipoifunga Steaua Bucharest, Jumamosi alifunga Bao.
Steaua Bucharest v Chelsea
Chelsea wamejitayarisha kwa Mechi hii kwa Jumamosi kutoka Sare ya 1-1 na Tottenham huku Straika wao Fernando Torres akitolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Hii ni Mechi ambayo hata Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amekiri hawatakiwi kuipoteza kwa vile walichapwa 2-1 na FC Basel katika Mechi ya kwanza ya Kundi hili.
Msimu uliopita Steaua iliifunga Chelsea 1-0 kwenye Raundi ya Mtoano ya EUROPA LIGI lakini wakachapwa 3-1 kwenye Marudiano huko Stamford Bridge.
KUNDI F
Arsenal v Napoli
Arsenal waliuanza Msimu huu kwa kuchapwa 3-1 na Aston Villa kwenye Ligi Kuu England lakini tangu hapo wameshinda Mechi 9 mfululizo na sasa wanaongoza Ligi hiyo na ushindi huo ni pamoja na kuifunga Ugenini Marseille Bao 2-1 kwenye Mechi ya kwanza ya Kundi hili.
Wikiendi hii iliyopita, Arsenal waliifunga Swansea City Bao 2-1 kwenye Ligi huku Kiungo wao Aaron Ramsey akifunga Bao na hiyo ni Gemu 4 mfululizo anapachika Mabao.
Rafael Benitez, aliewahi kuwa Meneja wa Liverpool na Chelsea, ndie aiongoza Napoli ambayo kwenye Serie A huko Italy inafanya vyema sana wakiwa wametoka Sare Mechi moja tu kati ya 6 walizocheza na wako Nafasi ya Pili, Pointi 2 nyuma ya Vinara AS Roma.
Jana Napoli walitangaza Kikosi chao ambacho kimetua London kuikabili Arsenal na nacho ni:
Makipa: Rafael, Reina, Colombo.
Mabeki: Albiol, Britos, Cannavaro, Fernandez.
Viungo: Armero, Behrami, Dzemaili, Hamsik, Inler, Mesto, Radosevic, Zuniga.
Mafowadi: Callejon, Mertens, Higuain, Insigne, Pandev, Duvan.
Borussia Dortmund v Marseille
Borussia Dortmund, ambao walifika Fainali ya Mashindano haya Msimu uliopita, wameanza vyema Bundesliga na kuongoza kwa kushinda Mechi 6 kati ya 7 na Jumamosi waliishindilia Freiburg Bao 5-0.
Lakini kwenye UCL kwenye Kundi hili wameanza vibaya kwa kufungwa 2-1 Ugenini na Napoli katika Mechi ambayo Kipa wao Roman Weidenfeller alitolewa kwa Kadi Nyekundu, hivyo hachezi Mechi hii, na pia Kocha wao Jurgen Klopp, kutolewa nje na Refa.
KUNDI G
Zenit Saint Petersbug v Austria Vienna
Timu zote hizi zimefungwa Mechi zao za kwanza kwa Zenit kufungwa Ugenini 3-0 na Atletico Madrid na Vienna kuchapwa Nyumbani kwao 1-0 na FC Porto.
Lakini Zenit, wakicheza Nyumbani ni wakali na ambako ndio wanaongoza Ligi ya Urusi na Juzi kuwafunga Spartak Moscow 4-2 huku Alexander Kerzhakov akipiga Bao lake la 208 kwenye Ligi na kumfanya awe Mfungaji Bora katika Historia ya Ligi ya Urusi.
Austria Vienna wapo Nafasi ya 5 kwenye Ligi ya kwao na walifungwa 1-0 na Admira hivi Juzi.
FC Porto v Atletico Madrid
Atletico Madrid wako moto huko kwao kwenye La Liga kwa kukamatana Pointi sawa na Vinara Barcelona na Juzi waliichapa Real Madrid 1-0, kwa Bao la Mbrazil Diego Costa, huko Santiago Bernabeu na kuua Rekodi ya kutoifunga Real kwenye Ligi kwa Miaka 14.
Hata hivyo, Atletico watatinga Mechi hii bila Diego Costa ambae anamalizia Kifungo chake cha Mechi za Ulaya 4.
Porto nao wanaongoza Ligi yao wakiwa Pointi 2 mbelle ya Sporting Lisbon huku kila Timu ikiwa imecheza Mechi 6.
KUNDI H
Ajax v AC Milan
Ajax wapo Nyumbani na katika Mechi ya kwanza ya Kundi hili walichapwa 4-0 Ugenini na Barcelona.
Ajax wamejitayarisha kwa Mechi hii kwa kuidunda Go Ahead Eagles Bao 6-0 kwenye Mechi ya Ligi ya kwao na kuwafanya wawe Pointi 1 nyuma ya Vinara PSV Eindhoven.
Nao AC Milan, ambao wameshinda Mechi 2 tu za Serie A kati ya 6 na wapo Nafasi ya 9, wanatinga kwenye Mechi hii wakiwa na Majeruhi kadhaa lakini walishinda Mechi yao ya kwanza ya Kundi kwa kuichapa Celtic 2-0.
Celtic v Barcelona
Msimu uliopita kwenye Hatua ya Makundi ya UCL, Celtic waliichapa Barcelona 2-1 ndani ya Celtic Park na leo Barcelona wanatinga tena bila ya Supastaa wao Lionel Messi ambae ni Majeruhi baada kuumia Jumamosi iliyopita kwenye Mechi ya La Liga walipoichapa Almeria 2-0.
RATIBA:
[Saa za Bongo]
Jumatano 2 Oktoba 2013
[Saa 1 Usiku]
PFC CSKA Moskva v FC Viktoria Plzeň
[Zote kuanza Saa 3 Dakika 45 Usiku]
FC Shakhtar Donetsk v Manchester United FC
Bayer 04 Leverkusen v Real Sociedad de Fútbol
Juventus v Galatasaray A.Ş.
Real Madrid CF FC København
Paris Saint-Germain v SL Benfica
RSC Anderlecht v Olympiacos FC
Manchester City FC v FC Bayern München

No comments:

Post a Comment

Adbox

@templatesyard