JUSTINE BIEBER AFURAHIA KUVUTA BANGI

kinda wa  muziki wa Pop Justine Bieber kwa nyingine amedai kuwa hakuna kitu ambacho kinampa raha kama kuvuta bangi.

Bieber aliyasema hayo nchini kwao Canada katika kituo kimoja cha televisheni ambapo mtangazaji alitaka kujua kama ni kweli anatumia kilevi hivyo.

Bila ya hata uwoga Bieber alimua kufunguka," Napenda kuvuta kwa kuwa ndio starehe ambayo inanipa raha kuliko vyote."

Hii ni mara ya pili katika nchi tofauti kwa kijana huyu ambaye yupo katika kilele cha mafanikio kukiri kutumia bangi.

Lakini watu wameonekana kuwa na mtazamo tofauti nchini kwao, huku wengi wakidai kipindi hicho kitachangia kuharibu watoto wengine kutokana na kutaka kuiga.

No comments:

Post a Comment

Adbox

@templatesyard