MTOTO ASHAMBULIWA VIBAYA MBELE YA POLISI

Mtoto Mitimo Clement(7)akitoa machozi baada ya kuzabuliwa makofi kichwani na mjomba wake anayehafamika kwa jina la Dickson Masabo(22)mbele ya askari Polisi katika Kituo Kipya cha mabasi mjini Tabora eti kwa kudaiwa kuwa mtoto huyo alikuwa akililia kusafiri na shangazi yake.Bw.Dickson na mkewe wakifurahia kitendo cha kumpiga makofi mtoto huyo mpaka kuanguka chini huku alama za vidole vya mkono wa Dickson vikibaki kwenye upande wa uso wa mtoto huyo vikiashiria maumivu makali kutokana na kipigo hicho kikali."Kwani vipi si nimempiga mimi ambaye ndiye ninamlea tatizo liko wapi?"Dickson alisikika akiwajibu askari Polisi walioshudia tukio hilo.Baadhi ya askari Polisi wa Kituo cha mabasi Tabora mjini wakiwa na mtoto huyo huku Dickson naye akiwekwa chini ya ulinzi mkali.Dickson akiwa chini ya ulinzi wa Polisi kutokana na tukio hilo la kibabe.

No comments:

Post a Comment

Adbox

@templatesyard